Ladislaus Fredrick alisema mpaka sasa tatizo utumikishwaji wa watoto hapa nchini bado halijafanyiwa utafiti Wa kutosha ili kuweza kubaini ukubwa Wa tatizo pamoja naathari zake.
Kwa upande wake Mratibu Wa mradi Wa WEKEZA Mkoa Wa Tanga Theresa Fovo alisema kuwa mradi huo umelenga kuhakikisha unatoa elimu Kwa jamii kuhusu kukomeshwa pamoja madhara ya ajira Kwa watoto.
“Theresa Fovo alisema mpaka sasa wamefanikiwa kufungua Club
za watoto
katika mashule wilayani Tanga, Muheza, na Korogwe ili kufwatilia na
kutoa takwimu mashuleni na zaidi ya watoto
4,000 wamefikiwa na kaya 1,680 na vijana 2,100 wameweza kunufaika na mradi wa
WEKEZA.
Pia washirika Semina walishukuru kwa mafunzo mazuri
ambayo wameyapata
yatasaidia sana katika kuelimisha jamii kupiga vita utumikishwaji wa
watoto kwani tatizo hili ni kubwa katika jamii na pia jamii haina elimu ya
kujua swala la utumikishwaji mtoto ni kosa kisheria.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni