

Walisema kuwa shule hiyo ambayo
imejengwa kwa nguvu za wananchi kwa lengo la kuwapunguzia kutembea umbali mrefu
wanafunzi wanaoishi katika mtaa huo.
Naye Saleh Gofa alisema kuwa ni vema Jiji
wakawaonyesha eneo jingine la kujenga shule kabla ya mradi haujaanza
kutekelezwa katika eneo hilo.
“Tunaiomba Halmashauri ya Jiji
itutafutie eneo jingine na kama kunauwezekano wa kujengewa shule nyingine
itakuwa vizuri zaidi kwani ya awali ilitokana na nguvu za wananchi
wenyewe”alisema Gofa.
Markus Tuwaya ameiomba Halmashauri
kuwasaidia kuwatafutia maeneo mengine ya makazi kwani kuna baadhi ya nyumba
zitabomolewa ili kupisha mradi pamoja na fidia ili waweze kuanza maisha mpya
tena bila ya kusuasua.
“Kunatabia imejengeka ikiwa wananchi
wanalipwa fidia bila ya kuonyeshwa maeneo mengine ya kuendeleza makazi tunapo
hamia wananchi wanatuuzia maeneo kwa gharama kubwa zaidi “alisema Tuwaya.
Hata Hivyo Mwenyekiti wa Mtaa huo
Said Kanuni alisema kuwa tayari taarifa za uwepo wa wananchi wanaohitaji fidia
ameshaziwasilisha kwa Mkurungenzi wa Jiji Daudi Mayeji kwa ajili ya taratibu
nyingine.
“Changamoto kubwa ni baadhi ya
wananchi hawana taarifa za kutosha kuhusu mfumo wa fidia watakao lipwa hivyo
husababisha kuwa na hofu ya kukosa fidia kabisa”alisema Kanuni.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni