WAKATI wafanyakazi wa Idara ya Afya Jiji la Tanga wakikazana kuliweka Jiji katika hali ya usafi imekuwa ni tofauti kwa soko
la Mgandini.
Akizungumza mmoja wa wafanyabiashara ambaye hakutaka jina
lake litajwe alisema kufanya usafi mara moja sio kumaliza uchafu, hali ya soka
inataka kufanyiwa usafi na kuzoa taka kila baada ya siku moja au mbili kwani ni
sehemu yenye watu wengi.
Halmashauri ya jiji la Tanga hufanya usafi katika mifereji
na masoko kila siku lakini inadaiwa kuwa usafi katika masoko bado kutakuwa kunaongeza
kasi kwa wafanyabiashara ili kutunza mazingira yao kuepuka miripuko ya
magonjwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni